Robertinho aitolea macho Al Ahly

© Kwa Hisani

KANDANDA Robertinho aitolea macho Al Ahly

Zahoro Mlanzi • 21:31 - 09.10.2023

Simba itashuka uwanjani Oktoba 20 kuumana na Al Ahly katika michuano hiyo na itarudiana baada ya siku nne jijini Cairo, Misri.

Baada ya kushinda mechi zao tano mfululizo za Ligi Kuu Bara, Kocha wa timu ya Simba SC, Robert Oliviera 'Robertinho', amesema kwa sasa wanaelekeza nguvu katika mchezo wao wa michuano ya African Super League (ASF).

Simba itashuka uwanjani Oktoba 20 kuumana na Al Ahly katika michuano hiyo na itarudiana baada ya siku nne jijini Cairo, Misri.

Kocha huyo ambaye ameingoza Simba kujikusanyia alama 15 na kuwa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo, amesema wanashukuru kutimiza malengo ya kushinda mechi zao mbili za ugenini.

"Nawashukuru wachezaji wangu na mashabiki zetu ambao wamekuwa wakitusapoti wakati wote, malengo yetu yalikuwa ni kushinda mechi hizi mbili za ugenini na hilo tumefanikiwa, hivyo tutaanza kujiandaa na mchezo ujao dhidi ya Al Ahly," amesema Robertinho.

Amesema Al Ahly ni timu kubwa barani Afrika hivyo hata maandalizi yake lazima yatakuwa tofauti na unavyojiandaa na ligi ya hapa nyumbani.

Katika hatua nyingine, klabu hiyo na Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), zimekubaliana kuendelea kushirikiana na kuipa fursa klabu hiyo ya kutumia huduma za ATCL.

Akizungumza baada ya kufanya ziara ya kuishukuru ATCL kwa uhusiano mzuri na Simba, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula amesema: “ATCL mmekuwa washirika muhimu sana kwenye mafanikio ya Klabu ya Simba kwa kutupa usafiri wa uhakika na bora kwa ajili ya timu yetu.

"Tukielekea kwenye mechi ya AFL dhidi ya Al-Ahly tufurahi kujua kwamba ATCL itakuwa mbia muhimu kusafirisha mashabiki kutoka sehemu mbalimbali kuja kuangalia mchezo huo.”

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Jamal Kiggundu, amesema:“ATCL inafurahi sana kuwa mbia wa Simba na iko tayari kufanya kazi pamoja na Simba katika kusafirisha timu na pia mashabiki.